Kipya kutoka Tecno: Phantom 8 na Phantom 8 Plus?

Mwandishi Diana Benedict

Mwisho wa mwaka Makampuni kama Apple, Samsung, HTC na Google walizindua vifaa vyao vipya kwa wateja wake. Kwa upande mwingine Kampuni inayoongoza kwa kuuza smartphone za bei nafuu Africa nayo inatarajia kuzindua vifaa vyake viwili  ifikapo Octoba 22 Dubai.

Mtaawasaba ilifanikiwa kuzipata taarifa hizo kupitia ukurasa wa Twitter wa @TECNOMobileNG na kupata baadhi ya picha za vifaa hivyo viwili Tecno Phantom 8 na Tecno Phantom 8 Plus.

Specification

By the way Hebu tuzingalizie bidhaa hizi mbili zitakuwa na kipi kipya zaidi?

Tecno Phantom 8 inatarajiwa kuwa na

  • Kioo cha 5.5 inch full HD display
  • 6GB RAM
  • 32GB or 64GB storage
  • 13MP + 5MP dual rear cameras (kama ilivyokuwa Phantom 6)
  • 8MP front camera
  • Mediatek Helio P25 Octa-core 2.6GHz Processor
  • 3500mAh battery
  • Android 7 Nougat utakayoweza kuupdate kwenda android 8 (Oreo)
  • Plastic Body

Na Tecno Phantom 8 Plus

  • Kioo cha 6.0 inch full HD display
  • 6GB RAM
  • 64GB storage
  • Mediatek Helio X30 Processor
  • 2x Telephoto Lens camera
  • 20MP front camera
  • 4000mAh battery
  • Android 7 Nougat (or some suggest Android 8 Oreo)
  • Body ya Metal au Glass
a01f8e12ec1324538612a3d1fd8a0a8b
Picha mojawapo ya Tecno Phantom 8 Iliyovuja mtanadoni

Hata hivyo Mtaawasaba haijathibisha kuwa ndio zitakuwa specification halisi ya simu hizo mbili.

Tufuatilie @MtaawaSaba ili usipitwe na Habari, Uchambuzi naMakala mbali mbali ya mitanadoni na ya kiteknolojia kwenye Facebook, Twitter, Instagram, Google+ na Youtube, Pia usisite kutoa maoni yako hapo chini au tuandikie barua pepe kwa [email protected]

Mwandishi Diana Benedict Mwandishi
Mitandao ya Kijamii
Diana Benedict. Digital Creator | IT Specialist | Graphics Designer | Web Designer | Web SEO | Contents Management | UI/UX Designer and Social Media Management.
Maoni yako

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive